FROM COAST

Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

RAIS JAKAYA KIKWETE AWASILI WASHINGTON DC‏


 Rais Dkt Jakaya Kiwete  akiingia Ritz Calton Hotel wakati alipowasili Washington, DC kwa kuendelea na ziara yake ya nchini Marekani aliyoanzia kwenye miji ya San Francisco na Vallejo, California.
 Rais Dkt Jakaya Kiwete akisalimiana na Mwambata mpya wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na Canada Kanali Adolph Mutta ambaye anachukua nafasi ya Brigedia Jenarali Emamanuel Maganga ambaye amemaliza muda wake.
 Rais Dkt Jakaya Kikwete akisalimiana na Afisa Ubalozi Emmanuel Swere kwenye hotel ya Ritz Calton wakati alipowasili Washington, DC.
 Rais Dkt Jakaya Kikwete akisalimiana na Afisa Ubalozi Catherine Kijuu.
 Rais Dkt Jakaya Kikwete akisalimiana na Mfanyakazi wa Ubalozi, Love Maganga.
 Rais Dkt Jakaya Kikwete akisalimiana na mfanyakazi wa Ubalozi, Mayor Mlima.
 Rais Dkt. Jakaya Kikwete akisalimiana na mfanyakazi wa Ubalozi Mariam Mkama.
 Rais Dkt. Jakaya Kikwete akisalimiana na mfanyakazi wa Ubalozi Carol Mbilinyi.
 Rais Dkt Jakaya Kikwete akisalimiana na mfanyakzi wa Ubalozi Rani Servin.
 Rais Dkt Jakaya Kikwete akisalimiana na mfanyakazi wa Ubalozi, Eliud Mbowe.
Balozi wa Heshima kutoka San Francisco California, Ahmed Issa akisalimiana na Afisa Ubalozi Suleiman Saleh aliyesimama kati ni Sherry Julian (mke wa Ahmed Issa).
Picha ya pamoja.
[ Read More ]

BINTI WA NIGERIA ATANGAZWA KUWA MISS WORLD MUSLIMAH 2013

Binti wa kinigeria Obabiyi Aishah Ajibola mwenye umri wa miaka 21, jana ametangazwa kuwa mshindi wa shindano la Miss World Muslimah wa mwaka 2013 lililofanyika mjini Jakarta,Indonesia.

Mabinti 20 kutoka nchi sita ndio waliofanikiwa kuingia fainali ambapo washiriki wote walivaa hijabu na mavazi yaliyostiri maungo yao. Baada ya kuonesha watazamaji na wasomi wa kiislamu, jopo la majaji lilimchagua Obabiyi Aishah Ajibola kutoka Nigeria kuwa mshindi. Vigezo vilivyotumika kumpata mshindi ni Ufasaha wa kusoma Qurani na Maoni yao juu ya Uislamu katika Dunia ya kisasa.

Baada ya kusikia jina lake kama mshindi Obabiyi Aishah Ajibola, alilia kwa furaha na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa yeye kuwa mshindi. “Jambo hili hasa si kushindana bali sisi tunajaribu tu kuonesha Dunia kwamba Uislamu ni mzuri” alisema Aishah.

Eka Shanti ambaye ndiye aliyeanzisha shindano hili miaka mitatu iliyopita, baada ya kupoteza kazi yake ya utangazaji wa Televisheni kwa kukataa kuvua Hijabu akiwa anatangaza, anasema, "Mwaka huu tumefanya makusudi lianze shindano letu kabla ya Miss World ili kuonesha kwamba kuna jambo mbadala na mfano wa kuigwa kwa wanawake wa kiislamu.”




Shindano hili lilianza mwaka 2011 likiwa na jina tofauti lilishirikisha waindonesia peke yake. Shanti anasema baada vyombo vya habari kulinganisha na Miss World tulibadilisha jina na tulikubali kuweka wagombea wa kigeni mwaka huu. Washiriki wa nje ya Indonesia, walitoka nchi za  Iran, Malaysia, Bangladesh, Brunei, na Nigeria.
Obabiyi Aishah Ajibola

Akivishwa Taji

Akivishwa beji ya Miss world Muslimah
Akishangilia kwa kushukuru baada ya kuangazwa mshindi

Washiriki wa Miss World Muslimah
[ Read More ]

LEADERSHIP MISTAKES THAT NO ONE WILL POINT OUT







Sure you are an excellent leader but you are not perfect. You may ask for feedback and work upon your flaws but there are a few things that no one will tell you. Whether they hope you will understand by yourself or whether they think it is too risky to point out, fact remains that there are some things that you should figure out yourself. Even a great number of aptitude tests will not tell you of these mistakes.
So, how do you figure out what these flaws are and how do you correct them? How do you understand what you are screwing up? Here are three things that many leaders screw up. Read and find out whether you have any of these bad qualities:

Family Issues:
It may be your uncle or your niece or your brother. Not many family members actually give in their hundred percent because they think they can get away with anything. Their brother/relative is the boss. They won’t be fired. So they can do whatever they want and get away with it. You might think you are doing justice to everyone and you might think your family members are doing their job. However, things are generally not like that. And this is something no one will ever dare tell you.
You should figure this out yourself through constant vigilance.

Arrogance:
Being aggressive is one thing. Being arrogant is extremely different. Aggression is good because it works as a drive at times. It motivates your employees to do better. It instills aggression in them too. However, arrogance will lead to your downfall. Thinking you are the best and you occupy the highest position in the world will just irritate your employees and make them less interested in working for you. There will be no motivation to work. They will work for the sake of it.
Obviously, no one will come and tell you that you should deflate your head a little.

Overstaying your Welcome:
Of course you should attend meetings but you shouldn’t overstay. After a point, your team wants to have some space to discuss things without you lurking over them. The same goes with projects. Some projects just don’t work no matter how long you stick to them. You should give up when you know it won’t be successful and concentrate on coming up with something better. Overdoing things will not help you at all. It is important to step aside and let others play a role even though you are qualified. It is important to give your team the flexibility to gather and discuss without you.
Of course, no one will dare tell you about this in his or her feedback.
These are mistakes that you should assess by yourself and rectify as soon as possible.

Entrepreneurial Learning:
There are a few things about you that you should understand yourself. There are a few mistakes that no one will point out. These include arrogance, overstaying, and family-related issues. Analyze your habits and be vigilant in order to know if you are committing any of these mistakes. If yes, it is time to rectify them immediately.


[ Read More ]

HAPPY BIRTHDAY NELSON MANDELA

 Nelson Rolihlahla Mandela.
 
LEO ni siku ya kuzaliwa kwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, Nelson Rolihlahla Mandela. Mzee Mandela ametimiza miaka 95 ya kuzaliwa mbali na afya yake kuwa mbaya baada ya kuwa mahututi kwa muda mrefu katika hospitali moja nchini Afrika Kusini. Tunamtakia kila la kheri Mzee Mandela katika siku yake ya kuzaliwa leo.

[ Read More ]

MAMA AMCHOMWA MWANAE NA MKASI MARA 90 KWA MADAI YAKUMG'ATA ZIWA AKIWA ANANYONYA.

Maskini unyama mwingine hauna hata maana maybe alikuwa amechanganyikiwa
Kweli ukistaajabu ya Musa....
Ni kama miujiza kwa mtoto wa kichina kuwa hai mpaka sasa licha ya kuchomwa chomwa mara 90 na mama yake mzazi huko China kwa madai kuwa alimng’ata ziwa mama yake wakati akinyonyeshwa.
Kwa mujibu wa Daily Mail mtoto huyo Xiao Bao mwenye miezi 8 tu ameshonwa zaidi ya nyuzi 100 ili kuurudisha uso wake katika hali nzuri baada ya shambulizi hilo lililotokea katika jiji la Xuzhou mashariki mwa China.
Bao anaishi na mama yake pamoja na wajomba zake wawili ambao wanajishughulisha na ukusanyaji wa taka kwaajili ya kipato. Mmoja wa wajomba hao ndiye aliyegundua kuwa Bao ameumizwa baada ya kumkuta akiwa amelala kwenye damu iliyotapakaa nyumbani hapo kabla hajamkimbiza hospitali
Mama wa mtoto huyo baadaye alikiri kumchoma choma mwanae na mkasi mara 90 hususan eneo la usoni baada ya mtoto huyo kumng’ata ziwa wakati akimnyonyesha.
Baada ya tukio hilo majirani wa familia hiyo wameiomba serikali imnyang’anye mama huyo wa kichina mtoto kwa sababu za kiusalama, lakini ombi hilo limekataliwa kwa madai kuwa hakuna uthibitisho wowote mpaka sasa kama mwanamke huyo anamatatizo ya akili, lakini wameongeza kuwa hata hivyo mtoto huyo bado ana walezi wengine wawili anaoishi nao (wajomba zake)
Mtoto huyo anaendelea kupata nafuu akiwa hospitali.

Source: Vijimamb
[ Read More ]

Kumbukumbu ya kutimiza miaka 13 ya kifo cha Baba yetu Mzee Mustafa Katuli.



Ni miaka kumi na tatu (13) tangu ututoke baba yetu mpendwa Mustafa Katuli.Unakumbukwa sana na watoto wako Farida,Othman,Maana,Khadija na Rehema. pia na Ndugu,jamaa na marafiki zako,Tulikupenda sana ila Mungu amekupenda zaidi. Allah akulaze mahala pema peponi. Amin.
[ Read More ]

Angelina Jolie akatwa matiti kuzuia Saratani


Angelina Jolie
Mcheza filamu mashuhuri sana duniani,Angelina Jolie amesema kwamba amekatwa matiti yake yote pamoja na kuondoa mfuko wake wa uzazi.
Kwenye taarifa aliyoandika kwenye gazeti la New York Times, Bi Jolie amesema alifanyiwa uchunguzi wa celi zake na kugunduliwa kwamba alikuwa katika hatari kubwa sana ya kupata saratani ya matiti. Ndipo akaamua kukatwa matiti yake mawili.
Angelina mwenye umri wa miaka 37 na mama na watoto sita, alipoteza mamake mzazi kutokana na maradhi ya saratani ya matiti.
Anasema aliandika taarifa hiyo kuwahakikishia watoto wake kwamba hakuwa kwenye hatari ya kupata saratani tena.
Kulingana na Jolie madaktari walisema kuwa uwezekano wake kupata Saratani ya matiti ni asilimia 87 huku akiwa na asilimia 50 uwezo wake wa kuugua Sarati ya mfuko wa uzazi.
''Niliamua kuchukua hatua mwenyewe ili kuzuia uwezekano wowote wa kuugua Saratani hiyo,'' alisema Jolie.
Alisema kuwa shughuli hii ilianza mwezi Februari na kukamilika mwishoni mwa mwezi April.

Uwezekano wapunguzwa.

Katika taarifa iliyoandikwa na Bi Jolie na yenye kichwa, 'Uamuzi wangu wa kimatibabu', Bi Jolie alieleza kuwa mamake alipambana na Saratani kwa miaka kumi na kufariki akiwa na umri wa miaka 56.
Alisema kuwa alielewa fika kuwa siku moja atawahi kuugua Saratani na ndio maana akachukua uamuzi wa kufanyiwa upasuaji huo mgumu wa wiki tisa ambao ulihitaji kukatwa matiti.
Angelina Jolie na Brad Pitt
Uwezekano wake wa kuugua saratani sasa umeshuka kutoka 87% hadi 5%.
Alimsifu mumewe Brad Pitt, kwa kumuunga mkono na kumfariji kwa kila aliyopitia, na kusema kuwa ametulizwa na kuwa wanawe hawakupata lolote katika matokeo ya uchunguzi wa madaktari tangu kufanyiwa upasuaji.
"ninahisi kuwa na nguvu kwa uamuzi niliofanya, na kwa kuwa ninasalia kuwa mwanamke hata baada ya kuondoa viungo hivyo,'' alisema Bi Jolie.
"kwa mwanamke yeyote anayesoma maneno haya, natumai ataweza kujua kuwa wanaweza kufanya uamuzi.''
Muigizaji huyo, ambaye ameshinda tuzo nyingi kwa uigizaji wake, pia ni mtunzi wa filamu na mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa anayehusika na harakati za kibinadamu.
Wakati alipokuwa anafanyiwa upasuaji, Bi Jolie alizuru Jamuhuri ya Kidremokrasia ya Congo pamoja na waziri wa mambo ya nje wa Uingereza William Hague.
Jolie pia alihudhuria mkutano wa mawaziri wa mambo ya nchi za kigeni wa G8, kuhamasisha dunia kuhusu dhulma za kingono katika maeneo ya vita.
[ Read More ]

Ujumbe wa Oman Wawasili Zanzibar kwa matayarisho ya Mkutano wa Kimataifa wa Historia ya Oman na Zanzibar, Historia ya Kiislam na Utamaduni wake.



Kaimu Balozi Mdogo wa Oman Zanzibar Saleh Suleiman, akisalimiana na Kiongozi wa Msafara wa Wajumbe wa Oman waliowasili Zanzibar leo kwa ajili ya matayarisho wa Mkutano wa Historia na Utamaduni wa Kiislam. unaotarajiwa kufanyika mwezi wa september 2013 Zanzibar. 
 BALOZI wa Oman  nchini Tanzania Yussuf Al Bakar ( katikati) akiongozana na Ujumbe kutoka Nchini Oman ukiwasili Zanzibar kwa ajili ya matayarisho ya Mkutano wa Kimataifa wa utakaozungumzia Historia na Utamaduni wa Kiislam Zanzibar kulia Kiongozi wa Ujumbe huo Dk. Hamed Mohammed Al Dhawiyaniy, ni Mwenyekiti wa Taifa wa Mamlaka ya Makumbusho ya Taifa ya Oman. Na kushoto Kaimu Balozi Mdogo wa Oman Zanzibar Saleh Suleiman

 Ujumbe wa Oman ukiwa katika ukumbi wa Wageni katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume wakibadilishana mawazo baada ya kuwasili Zanzibar leo.
Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Dkt. Haji Mwevura Haji,akizungumza katika mkutano na Ujumbe wa Oman, uliowasili Zanzibar kwa matayarisho ya mkutano wa Historia na Utamaduni wa Kiislam, kushoto Dk. Hamed Mohammed Al Dhawiyaniy, ni Mwenyekiti wa Taifa wa Mamlaka ya Makumbusho ya Taifa ya Oman,na kulia Mkurugenzi Mkuu wa Kitengo cha Historia ya Uislam Oman Dkt.Halit Eren.
 Mkuu wa Msafara wa Ujumbe wa Oman uliowasili Zanzibar kwa matayarisho wa Mkutano wa Kimataifa utakaozungumzia Historia na Utamatudi wa Kiislam, Dk. Hamed Mohammed Al Dhawiyaniy, ni Mwenyekiti wa Taifa wa Mamlaka ya Makumbusho ya Taifa ya Oman,Zanzibar ina mahusiano ya Kihistoria na Mataifa ya Kiarabu katika historia na Utamaduni wa Kiislam.kulia  Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Dkt. Haji Mwevura Haji na  Mkurugenzi Mkuu wa Kitengo cha Historia ya Uislam Oman Dkt.Halit Eren,
 Mkuu wa Skuli ya Kiswahili na Lugha za Kigeni Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar Dkt. Issa Haji Zidi, akitafsiri katika mkutano huo kutoka katika lugha ya Kiarabu, wakati wa mkutano huo wa matayarisho ya Mkutano wa Kimataifa wa Historia na Utamaduni wa Kiislam unaotarajiwa kufanyika Zanzibar mwezi wa September 2013.  
 Mkurugenzi Mkuu wa Kitengo cha Historia ya Uislam Oman Dkt.Halit Eren, akizungumza katika mkutano huo uliowashirikisha Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar SUZA,  
 Ujumbe wa Oman wakimsikiliza Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Dkt. Haji Mwevura Haji, akizungumza katika mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa SUZA Majestiki Zanzibar. 
Ujumbe wa SUZA wakiwa katika Mkutano na Ujumbe kutoka Oman uliofika Zanzibar kwa maandalizi ya Mkutano wa Kimataifa wa Historia ya Uislam na Utamaduni wake baina ya Nchi hizi mbili.mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa mkutano Chuo Kikuu cha Taifa Kampasi ya Majestic Zanzibar. 
[ Read More ]

MAELFU WAHUDURIA MAZIKO YA MAREHEMU BI KIDUDE.

Jeneza la bibi likielekea msikiti kwa ajili ya kusaliwa
Mtangazaji Hassan Bond, Fid Q, Diamond Platnumz na Ruge Mutahaba wakiwa msibani nyumbani kwamarehemu bi Kidude,  Zanzibar

Msanii Fid Q, Baraka cousin ya Marehemu Bi Kidude na Hassan Bond Mussa (FID Q ndo alikuwa msanii wa kwanza mkubwa kufika msibani kwa bibi)
Ruge mutahaba, Babu Tale and Guru. .......msibani kwa Bi Kidude
Guru G na Mh Bhaa mazikoni
Hassan na Fid Q wakiwa katika picha ya pamoja na familia ya Marehemu Bi Kidude

Sehemu ya umati wa Watu waliofika msibani

Endelea kuwa nasi kwa tukio zima la maziko ya Bibi yetu
[ Read More ]

Bi Kidude Wakati wa Uhai wake



BiKidude akiwa katika viwanja vya Ngome Kongwe wakati wa Tamasha la Sauti za Busara 
 BiKidude akipinga ngoma aina ya Uyango katika matamasha yanayofanyika Zanzibar katika viwanja vya Ngomekongwe
 Mwaka 2005 huko Gateshead, Newcastle nchini Uingereza,Bi.Kidude alipokea tuzo yenye heshima kutoka World Music Expo (WOMEX) kwa mchango wake katika muziki na utamaduni wa Zanzibar. Katika kinyang’anyiro hicho aliwashinda wanamuziki mahiri kama Peter Gabriel, Miriam Makeba na wengineo. Bi.Kidude anasema hawezi kuacha kuimba mpaka siku atakapoiaga dunia kwani akiimba anajihisi kuwa binti wa miaka 14!


Mwaka jana, kampuni ya nchini Uingereza iitwayo ScreenStation kwa kushirikiana na Busara Promotions walitoa documentary iitwayo “As Old As My Tongue-The Myth and Life of Bi.Kidude” inayoelezea historia nzima ya maisha yake. Unaweza kuona dakika kama saba hivi za documentary hiyo hapa chini.Anasema yeye anakunywa na pia anavuta,lakini zaidi ya yote anaweza kuimba bila hata kutumia spika ya mdomo yaani microphone.
Picha hii ni kwa hisani ya Marcel Mutsaers aliyompiga Bi.Kidude wakati wa Tamasha lijulikanalo kama Festival Mundial kule Tilburg-Uholanzi mwezi June mwaka 2006.


Umri wake halisi haujulikani. Kinachojulikana ni kwamba ana umri zaidi ya miaka 90 na hivi sasa sio ajabu akawa ameshafikisha umri wa miaka 100! Amekuwa muimbaji tangu miaka ya 1920 akiwa ni mfuasi wa Sitti Bin Saad mmojawapo wa waimbaji wa mwanzo kabisa wa taarabu visiwani Zanzibar.

Hivi leo anatambulika na kuheshimika kama malikia wa taarabu na mambo ya unyago asiye na mpinzani. Alizaliwa katika kijiji cha Mfagimaringo katika familia ya watoto saba. Jina alilopewa na wazazi wake alipozaliwa ni Fatuma Binti Baraka kabla jina maarufu la Bi.Kidude halijashika baadaye alipoanza kuwa maarufu katika uimbaji.Wazazi wake walikuwa ni wafanyabiashara ya kuuza nazi enzi hizo za Zanzibar iliyokuwa chini ya utawala wa wakoloni.

Katika mahojiano mbalimbali aliyofanya na vyombo tofauti tofauti vya habari ulimwenguni Bi.Kidude anasema alianza kuimba akiwa na umri mdogo wa miaka 10. Anasema uimbaji alijifunza kutoka kwa Sitti binti Saad tena kwa kujificha nje ya nyumba na kumsikiliza Sitti binti Saad akiwaimbia wageni ambao mara nyingi walikuwa wakipelekwa pale na yeye Bi.Kidude.

Akiwa na umri wa miaka 13 tu hakuwa na jinsi bali kukimbilia Tanzania bara(Tanganyika enzi hizo) ili kuepuka kuozeshwa kwa nguvu. Akiwa Tanzania bara alizunguka kila kona ya nchi akiwa muimbaji katika makundi mbalimbali ya muziki wa taarabu likiwemo lile maarufu la Egyptian Musical Taarab. Baadaye alihamia nchini Misri kwa kifupi kabla hajarejea kisiwani Zanzibar mahali ambapo anaishi mpaka hivi leo.

Mbali na uimbaji Bi.Kidude pia ni mfanyabiashara.Anauza “wanja” na “hina” ambazo anazitengeneza mwenyewe. Pia ni mtaalamu wa dawa za mitishamba lakini zaidi ya yote yeye ni Mwalimu wa “unyago” ambapo anacho chuo chake mwenyewe huku akijivunia rekodi kwamba katika wanafunzi wake wote hakuna ambaye ameshawahi kupewa talaka na mumewe. Pengine hii ndio sababu mwaka 2004 ulipozuka umbea kwamba Bi.Kidude amefariki dunia wakati alipokuwa katika ziara ndefu ya kimuziki Ulaya na Mashariki ya mbali, kila mtu kisiwani Zanzibar alishikwa na butwaa na majonzi! Kwa bahati nzuri habari za “kifo” chake zilikuwa ni uzushi tu.
[ Read More ]